Chama cha upinzani nchini Tanzania Chadema, kimeishauri serikali ya nchi hiyo kuchukua hatua za kupunguza gharama za maisha hasa katika kipindi hiki ambacho bei za mafuta zimepanda.
Mjumbe wa kamati kuu ya Chadema John Heche amesema, kupanda kwa bei za mafuta haisababishwi na vita vitavyoendelea kati ya Urusi na Ukraine
Katika mkutano na waandishi wa habari ulifanyika hii leo jijini Dodoma, Bw. Heche, ameitaka serikali kuchukua hatua, kupunguza angalau shilingi 600 kwa kila lita ya mafuta.
Heche pia, ameishauri serikali kupunguza baadhi ya matumizi ambayo sio ya lazima kama sehemu ya kupunguza gharama za maisha.
‘’Katika mojawapo ya hatua za kukabiliana na ongezeko la bei za mafuta hapa nchini, Serikali imetoa ruzuku ya Shilingi billioni 100 kwa mwezi Julai mwaka 2022 ambayo imeelekezwa katika udhibiti wa bei ya mafuta ya petroli na dizeli ili kukabiliana na mfumko wa bei,’’alisema.
Kwa mujibu wa ofisi ya taifa ya takwimu Mfumko wa Bei wa Taifa kwa miezi kadhaa iliyopita, unaonekana kuongezeka hadi asilimia 3.8 kutoka asilimia 3.6.

0 Comments