Shirika la Afya Duniani linaonya kuwa Afrika inakabiliwa na hatari inayoongezeka ya milipuko ya magonjwa ambayo huenea kutoka kwa wanyama hadi kwa watu.
Linasema milipuko ya magonjwa ya aina hiyo imeongezeka kwa zaidi ya 60% katika muongo uliopita na kiwango kikubwa kilirekodiwa tangu 2019.
Visa vingi vimehusisha virusi vya Ebola, magonjwa mengine ya virusi ya kuvuja damu, homa ya dengue, kimeta na tumbili.
Mkurugenzi wa WHO kanda ya Afrika Matshidiso Moeti alisema kuna haja ya kuchukua hatua sasa kukomesha Afrika kuwa kitovu cha magonjwa ya kuambukiza yanayoibuka.
WHO inasema miongoni mwa sababu zinazochangia kuenea kwa magonjwa hayo ni ongezeko la kasi la watu, ongezeko la mahitaji ya chakula kinachotokana na wanyama na uvamizi wa makazi ya wanyamapori.

0 Comments